| |||||||||||||
| |||||||||||||
|
|||||||||||||
| AINA ZA HATARI / MFIDUO | MADHARA YA PAPO HAPO / DALILI | KINGA | HUDUMA YA KWANZA / UZIMAJI MOTO |
| MOTO |
Kilipukaji. Hutoa moshi (au gesi) wenye kukereketa au wenye sumu ukiwa motoni.
|
Usiwashe moto, usiwashe cheche, usivute sigara.
|
Poda, mnyunyizo wa maji, povu, dioksidi kaboni. Ondoa watu wote na uzime moto kutoka mahali inayostahimili mlipuko.
|
| MLIPUKO |
Hatari ya moto na mlipuko.
|
Zuia mlimbiko wa chaji za umemetuamo (k.m. kwa kutuliza). Tumia vifaa vya mkono visivyotoa cheche. USIACHE kikaathiriwa na msuguano au mshtuko.
|
Utokeapo moto: poza mapipa n.k. kwa kunyunyizia maji BILA (vilivyomo) kugusa maji. Zima moto ukiwa mahali pa usalama.
|
| MFIDUO |
|
FUATA MASHARTI YA AFYA KIKAMILIFU!
|
|
| Kuvuta pumzi |
Kuumwa kichwa. Kizunguzungu. Kichefuchefu. Udhaifu. Kujisikia joto na kujaa usoni. Maumivu kifuani. Dalili zinaweza kuchelewa (tazama Vidokezo).
|
Uingizaji hewa, mtambo wa kutolea nje, au kinga ya kupumulia.
|
Hewa safi, mapumziko. Mpeleke kwa matibabu.
|
| Ngozi |
YAWEZA KUFYONZWA! (Tazama Kuvuta pumzi).
|
Glavu za kinga. Mavazi ya kinga.
|
Vua nguo zilizosibikwa. Suuza na kisha safisha ngozi kwa maji na sabuni. Mpeleke kwa matibabu.
|
| Macho |
|
Kingao cha uso, au kinga ya macho pamoja na kinga ya kupumulia.
|
Kwanza safisha macho vizuri kwa dakika chache (ondoa lenzi mboni kama inawezekana kuziondoa kwa urahisi), kisha mpeleke kwa daktari.
|
| Kumeza |
(Tazama Kuvuta pumzi).
|
Usile, usinywe wala kuvuta sigara ukiwa kazini. Nawa mikono kabla ya kula.
|
Sukutua kinywa. Mtapishe (MTU MWENYE FAHAMU TU!). Mpeleke kwa daktari.
|
| KUSAFISHA MWAGIKO | UFUNGASHAJI / UWEKAJI LEBO | |||||||
|
Ondoka katika eneo la hatari. Shauriana na mtaalam. Kusanya kioevu kinachovuja na kilichomwagika katika vyombo vilivyozibwa kadri inavyowezekana. Fyonza kioevu kilichosalia katika mchanga au kifyonzi ajizi na kisha peleka mahala pa usalama. Usiruhusu kemikali hii iingie katika mazingira. (Kinga ya ziada ya binafsi: nguo kamili za usalama pamoja na vifaa vya kupumulia vilivyo toshelevu).
|
Usisafirishe pamoja na vyakula au malisho. Ainisho ya EU Alama: E, T+ R: 2-26/27/28-33 S: (1/2-)-33-35-36/37-45 Ainisho ya UN | |||||||
| HATUA ZA HARAKA | UHIFADHI | |||||||
|
|
Isodhurika kwa moto. Hifadhi kwenye jengo lililotengwa. Kinachotenganishwa na asidi, vyakula na malisho. Baridi. Kilichofungwa vizuri.
| |||||||
| ||||||||
| |||
| DATA MUHIMU | |||
|
HALI MAUMBILE; INAVYOONEKANA: KIOEVU KISICHO RANGI HADI MANJANO, KAMA MAFUTA HATARI ZA KIKEMIKALI: Kukanza kunaweza kusababisha mwako au mlipuko mkali kutoa mafusho yenye sumu (oksidi za nitrojeni). Huweza kutengana kwa mlipuko kutokana na mshtuko, msuguano, mtikiso. Humenyuka pamoja na asidi. VIKOMO VYA MFIDUO WA KAZI (OELS): TLV: 0.05 ppm; (as TWA) (ngozi) (ACGIH 1999) |
NJIA ZA MFIDUO: Dutu hii huweza kufyonzwa ndani ya mwili kwa kuvuta pumzi ya erosoli yake, kupitia kwenye ngozi na kwa kumeza. HATARI ZA KUVUTA PUMZI: Ukolezi unaodhuru unaweza kufikiwa haraka kutokana na uvukizi wa dutu hii ifikapo 20°C. ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MFUPI: Dutu hii huweza kuathiri mfumo wa moyo na mishipa, kusababisha nguvu ya damu kupungua kwa kasi. Dutu hii huweza kuathiri damu, kusababisha kufanyika kwa methemoglobini. Uchunguzi wa kitibabu unahitajika. Athari zinaweza kuchelewa. ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MREFU AU UNAORUDIWA: Kuwa nayo kila mara huleta mazoea. Lakini kusiokuwako kwa muda mfupi yaweza kusababisha kifo kwa ghafula. | ||
| TABIA ZA KIMAUMBILE | |||
|
Kiwango mchemko: hulipuka ifikapo 114°C Kiwango myeyuko: -22°C Uzito wiani (maji = 1): 1.49 Umumunyifu katika maji, g/100 ml ifikapo 25°C: 0.5 Kanieneo mvuke, Pa ifikapo 20°C: 7 Uzitowiani wa mvuke (hewa = 1): 5.2 |
Uzito wiani wa mvuke/hewa mahuluti ifikapo 20°C (hewa = 1): 1.0 Oktanoli/kizigeu mgawo cha maji kwa logi Pow: 1.16 | ||
| DATA YA MAZINGIRA | |||
|
Dutu hii inadhuru kwa viumbe viishivyo majini.
| |||
| VIDOKEZO | |||
|
Dalili kama kuumwa kifua, kupiga moyo kwa nguvu inayojia wakati hauko kwa kazi ni dalili ya kiwango cha sumu ya dutu hii na lazima ijulishwe kwa daktari anayehusika. Matumizi ya vileo huongeza athari zinazodhuru. Suuza nguo zilizosibikwa (hatari ya moto) kwa maji mengi. Usichukue nguo za kazi nyumbani. Kutegemeana na kiasi cha mfiduo, upimaji wa kitibabu wa mara kwa mara unahitajika. Matibabu mahsusi yanahitajika iwapo kuna uligaji kutokana na dutu hii; njia muafaka pamoja na maelekezo sharti yapatikane.
| |||
| MAELEZO YA ZIADA | |||
|
| |||
| |||
| © IPCS, CEC 2005 | |||