| ||||||||||||||
| ||||||||||||||
|
||||||||||||||
| AINA ZA HATARI / MFIDUO | MADHARA YA PAPO HAPO / DALILI | KINGA | HUDUMA YA KWANZA / UZIMAJI MOTO |
| MOTO |
Michanganyiko ya vioevu vyenye vimumunyisho vya kaboni huweza kuwaka (moto). Hutoa moshi (au gesi) wenye kukereketa au wenye sumu ukiwa motoni.
|
|
Povu, poda kavu, dioksidi kaboni, USITUMIE maji.
|
| MLIPUKO |
Madhara ya mlipuko yanategemea kimumunyisho kilichotumika katika utengezaji.
|
|
Utokeapo moto: poza mapipa n.k. kwa kunyunyizia maji BILA (vilivyomo) kugusa maji.
|
| MFIDUO |
|
FUATA MASHARTI YA AFYA KIKAMILIFU!
|
KWA HALI YOYOTE MWONE DAKTARI!
|
| Kuvuta pumzi |
|
Kinga kiambo ya utoaji moshi au kupumua.
|
Hewa safi, mapumziko.
|
| Ngozi |
YAWEZA KUFYONZWA! Wekundu.
|
Glavu za kinga. Mavazi ya kinga.
|
Vua nguo zilizosibikwa. Suuza na kisha safisha ngozi kwa maji na sabuni.
|
| Macho |
Wekundu.
|
Miwanivuli ya usalama. Kingao cha uso.
|
Kwanza safisha macho vizuri kwa dakika chache (ondoa lenzi mboni kama inawezekana kuziondoa kwa urahisi), kisha mpeleke kwa daktari.
|
| Kumeza |
Degedege. Kizunguzungu. Kichefuchefu. Kutapika.
|
Usile, usinywe wala kuvuta sigara ukiwa kazini.
|
Mpe tope chujio la mkaa ulioamilishwa katika maji anywe. Mtapishe (MTU MWENYE FAHAMU TU!). Kupumzika. Mpeleke kwa daktari.
|
| KUSAFISHA MWAGIKO | UFUNGASHAJI / UWEKAJI LEBO | |||||||
|
Usielekeze kwenye mfereji wa maji machafu. Zoa dutu iliyomwagiga katika vyombo vinavyokalafatika; endapo inafaa, loanisha kwanza ili kuzuia vumbi. Kusanya salio kwa uangalifu, kisha peleka mahala pa usalama.
|
Usisafirishe pamoja na vyakula au malisho. Kichafuzi cha maji/bahari. Ainisho ya EU Alama: T R: 23/24/25-36/38 S: (2-)-13-44 Ainisho ya UN Ainisho ya UN ya Hatari: 6.1 | |||||||
| HATUA ZA HARAKA | UHIFADHI | |||||||
|
Kadi ya Dharura ya Usafiri: TEC(R) - 61G53b
|
Hatari ya kuzuia mmiminiko kutoka kwenye kizimamoto. Kinachotenganishwa na vyakula na malisho. Weka gizani.
| |||||||
| ||||||||
| |||
| DATA MUHIMU | |||
|
HALI MAUMBILE; INAVYOONEKANA: MANGO MANJANO KAMA NTA YENYE HARUFU TAMBULISHI. HATARI ZA KIKEMIKALI: Dutu hii hutengana inapokanzwa, inapochomwa na/au inapoathiriwa na alkali, miale yenye nguvu na vichocheo vya metali, kama feri huzalisha mafusho yenye sumu. Hushambulia chuma. Haipatani na kiuadudu ya alkali. VIKOMO VYA MFIDUO WA KAZI (OELS): TLV: 0.5 mg/m³ (kama TWA) (ngozi) (ACGIH 1997) TLV (kama STEL): 1 mg/m³ (ngozi) (ACGIH 1997) |
NJIA ZA MFIDUO: Dutu hii huweza kufyonzwa ndani ya mwili kupitia kwenye ngozi na kwa kumeza. ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MFUPI: Dutu hii inakera kwa upole ngozi. Dutu hii huweza kuathiri mfumo mkuu wa neva kusababisha tetemeko na degedege. Mfiduo wa viwango vya juu huweza kusababisha kifo. ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MREFU AU UNAORUDIWA: Dutu hii ina uwezekano wa kusababisha kansa kwa binadamu. | ||
| TABIA ZA KIMAUMBILE | |||
|
Kiwango myeyuko: 65-90°C Uzito wiani (maji = 1): 1.65 Umumunyifu katika maji: hakuna Kanieneo mvuke, Pa ifikapo 25°C: 53 Uzitowiani wa mvuke (hewa = 1): 14.3 |
Oktanoli/kizigeu mgawo cha maji kwa logi Pow: 3.3 | ||
| DATA YA MAZINGIRA | |||
|
Dutu hii inaweza kuwa na madhara kwa mazingira; tahadhari maalumu itolewe kwa viumbe hai vya majini, viumbe vya ardhini, na ndege. Kuzidisha kwa kemikali yaweza kutokea viumbe vya majini.
| |||
| VIDOKEZO | |||
|
Hutengana ikikaribia kuchemuka. Camphechlor ni mchanganyiko wa kamfeni za klorini, ina klorini 67-69%. Kutumika kwa kiuadudu ya faa isitumike isipokuwa kama hakuna lingine. Kutegemeana na kiasi cha mfiduo, upimaji wa kitibabu wa mara kwa mara pendekeza. Vimumunyishaji chukuzi vitumikavyo katika misombo ya kibiashara vyaweza kubadilisha tabia za kimaumbile na za kitoksini. Usichukue nguo za kazi nyumbani. Alltox, Chem-Phene, M 5055, Clor Chem T-590, Crestoxo, Estonox, Fasco-Terpene, Geniphene, Gy-phene, Hercules 3956, Melipex, Penphene, Phenacide, Phenatox, Strobane-T, Toxakil, Toxyphene, Toxon 63 ni majina ya kibiashara.
| |||
| MAELEZO YA ZIADA | |||
|
| |||
| |||
| © IPCS, CEC 2005 | |||