| ||||||||||||||
| ||||||||||||||
|
||||||||||||||
| AINA ZA HATARI / MFIDUO | MADHARA YA PAPO HAPO / DALILI | KINGA | HUDUMA YA KWANZA / UZIMAJI MOTO |
| MOTO |
Huwaka.
|
Usiwashe moto.
|
Poda, povu linalokinza alkoholi, mnyunyizo wa maji, dioksidi kaboni.
|
| MLIPUKO |
Mvuke/hewa mahuluti inayolipuka huweza kufanyika inapovuka 65°C.
|
Mfumo funge wa zaidi ya 65°C, uingizaji hewa.
|
|
| MFIDUO |
|
|
|
| Kuvuta pumzi |
Kikohozi. Kuhara. Kizunguzungu. Kuumwa kichwa. Kichefuchefu. Kukosa pumzi. Kuumwa koo. Kufanyiza kisauti wakati wa kupumua.
|
Uingizaji hewa, mtambo wa kutolea nje, au kinga ya kupumulia.
|
Hewa safi, mapumziko. Mkao wa nusu wima. Mpeleke kwa matibabu.
|
| Ngozi |
YAWEZA KUFYONZWA! Ngozi kavu. Wekundu.
|
Glavu za kinga. Mavazi ya kinga.
|
Vua nguo zilizosibikwa. Suuza ngozi kwa maji mengi au oga.
|
| Macho |
Wekundu. Maumivu.
|
Miwanivuli ya usalama, kingao cha uso, au kinga ya macho pamoja na kinga ya kupumulia.
|
Kwanza safisha macho vizuri kwa dakika chache (ondoa lenzi mboni kama inawezekana kuziondoa kwa urahisi), kisha mpeleke kwa daktari.
|
| Kumeza |
Mchomo. Kuumwa kichwa. Kichefuchefu. Kupoteza fahamu.
|
Usile, usinywe wala kuvuta sigara ukiwa kazini.
|
Sukutua kinywa. Mpe tope chujio la mkaa ulioamilishwa katika maji anywe. Mpeleke kwa daktari.
|
| KUSAFISHA MWAGIKO | UFUNGASHAJI / UWEKAJI LEBO | |||||||
|
Kusanya kioevu kinachovuja na kilichomwagika katika vyombo vilivyozibwa kadri inavyowezekana. Osha salio kwa maji mengi. (Kinga ya ziada ya binafsi: kipumulio chujio cha gesi na mivuke ya kikaboni).
|
Usisafirishe pamoja na vyakula au malisho. Ainisho ya EU Alama: Xn R: 20/21/22 S: (2-) Ainisho ya UN Ainisho ya UN ya Hatari: 6.1 Kikundi Ufungashaji cha UN: III | |||||||
| HATUA ZA HARAKA | UHIFADHI | |||||||
|
Kadi ya Dharura ya Usafiri: TEC(R) - 61G61c Msimbo wa NFPA : H 1; F 2; R 1; |
Kinachotenganishwa na vioksidishaji vikali, asidi kali, vyakula na malisho.
| |||||||
| ||||||||
| |||
| DATA MUHIMU | |||
|
HALI MAUMBILE; INAVYOONEKANA: KIOEVU KISICHO RANGI, CHENYE HARUFU TAMBULISHI. HUGEUKA NYEKUNDU AU KAHAWIA INAPOFIDULIWA NA MWANGA NA HEWA. HATARI ZA KIKEMIKALI: Dutu hii hupolimisha kwa kuathiriwa na asidi. Humenyuka kwa ukali sana ikiwa na vioksidishaji vikali au asidi kali kusababisha athari ya moto na mlipuko. VIKOMO VYA MFIDUO WA KAZI (OELS): TLV: 10 ppm; 40 mg/m³ (kama TWA), 15 ppm; 60 mg/m³ kama (STEL) (ngozi) (ACGIH 1997). MAK: 10 ppm; 40 mg/m³; (1996). |
NJIA ZA MFIDUO: Dutu hii huweza kufyonzwa ndani ya mwili kwa kuvuta pumzi, kupitia kwenye ngozi na kwa kumeza. HATARI ZA KUVUTA PUMZI: Ukolezi unaodhuru waweza kufikiwa polepole kutokana na uvukizi wa dutu hii ifikapo 20°C. ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MFUPI: Inayotoza machozi. Dutu hii inakera macho, ngozi na njia ya upumuaji. Mfiduo juu zaidi ya OEL husababisha kupungua fahamu. ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MREFU AU UNAORUDIWA: Kioevu hukausha ngozi. Dutu hii huweza kuathiri mfumo mkuu wa neva. | ||
| TABIA ZA KIMAUMBILE | |||
|
Kiwango mchemko: 170°C Kiwango myeyuko: -15°C Uzito wiani (maji = 1): 1.13 Umumunyifu katika maji: kuchanganyika Kanieneo mvuke, Pa ifikapo 20°C: 53 Uzitowiani wa mvuke (hewa = 1): 3.4 |
Uzito wiani wa mvuke/hewa mahuluti ifikapo 20°C (hewa = 1): 1.00 Kiwango cha kumweka: 65°C c.c. 75°C o.c. Jotoridi la kujiwasha: 491°C Vikomo vya kilipukaji, % ujazo katika hewa: 1.8-16.3 Oktanoli/kizigeu mgawo cha maji kwa logi Pow: 0.28 | ||
| DATA YA MAZINGIRA | |||
|
| |||
| VIDOKEZO | |||
|
Viwango myeyuko vinginevyo: -31°C. Onyo la harufu wakati kikomo thamani cha mfiduo kinapovukwa halitoshi.
| |||
| MAELEZO YA ZIADA | |||
|
| |||
| |||
| © IPCS, CEC 2005 | |||