| ||||||||||||||
| ||||||||||||||
|
||||||||||||||
| AINA ZA HATARI / MFIDUO | MADHARA YA PAPO HAPO / DALILI | KINGA | HUDUMA YA KWANZA / UZIMAJI MOTO |
| MOTO |
Huwaka.
|
Usiwashe moto.
|
Poda, mnyunyizio wa maji, povu, dioksidi kaboni.
|
| MLIPUKO |
Mvuke/hewa mahuluti inayolipuka huweza kufanyika inapovuka 80°C. Chembechembe zilizotawanyika hufanya mchanganyiko ulipukao hewani.
|
Zuia utuaji wa vumbi; mfumo funge, vifaa vya umeme na taa visivyolipuka kwa vumbi.
|
|
| MFIDUO |
|
ZUIA MTAWANYIKO WA VUMBI!
|
|
| Kuvuta pumzi |
Kuumwa kichwa. Udhaifu. Kichefuchefu. Kutapika. Kutokwa jasho. Kuchanganyikiwa. Manjano ya macho na ngozi. Mkojo kuwa rangi ya udhurungi.
|
Uingizaji hewa (hapana kama ni poda), mtambo wa kutolea nje, au kinga ya kupumulia.
|
Hewa safi, mapumziko. Mpeleke kwa matibabu.
|
| Ngozi |
YAWEZA KUFYONZWA! (Zaidi tazama Kuvuta pumzi).
|
Glavu za kinga.
|
Suuza ngozi kwa maji mengi au oga.
|
| Macho |
|
Miwani ya usalama.
|
Kwanza safisha macho vizuri kwa dakika chache (ondoa lenzi mboni kama inawezekana kuziondoa kwa urahisi), kisha mpeleke kwa daktari.
|
| Kumeza |
Maumivu ya tumbo. Kuhara. Degedege. Kupoteza fahamu. (Zaidi tazama Kuvuta pumzi).
|
Usile, usinywe wala kuvuta sigara ukiwa kazini. Nawa mikono kabla ya kula.
|
Kupumzika. Mpeleke kwa daktari.
|
| KUSAFISHA MWAGIKO | UFUNGASHAJI / UWEKAJI LEBO | |||||||
|
Kinga ya ziada ya binafsi: kipumulio chujio cha gesi na mivuke ya kikaboni. Usiruhusu kemikali hii iingie katika mazingira. Zoa dutu iliyomwagiga katika vyombo vilivyofunikwa; endapo inafaa, loanisha kwanza ili kuzuia vumbi. Kusanya salio kwa uangalifu, kisha peleka mahala pa usalama.
|
Usisafirishe pamoja na vyakula au malisho. Kichafuzi cha maji/bahari. Ainisho ya EU Alama: Xn, N R: 22-40-50/53 S: (2-)-36/37-46-60-61 Ainisho ya UN Ainisho ya UN ya Hatari: 4.1 Kikundi Ufungashaji cha UN: III | |||||||
| HATUA ZA HARAKA | UHIFADHI | |||||||
|
Kadi ya Dharura ya Usafiri: TEC(R) - 41S1334 (mango); 41GF1-II+III (mango); 41S2304 (myeyuko) Msimbo wa NFPA: H 2; F 2; R 0; |
Kinachotenganishwa na vioksidishaji vikali, vyakula na malisho. Hifadhi mahali pasipokuwa na unyevu au uchafu.
| |||||||
| ||||||||
| |||
| DATA MUHIMU | |||
|
HALI MAUMBILE; INAVYOONEKANA: MANGO NYEUPE KATIKA MAUMBO MBALIMBALI YENYE HARUFU TAMBULISHI. HATARI KWA MWILI: Mlipuko wa vumbi huweza kutokea iwapo katika umbo la poda au punjepunje, vikichanganywa na hewa. HATARI ZA KIKEMIKALI: Inapowaka hutengeneza gesi zenye sumu na zinazowasha. Humenyuka pamoja na vioksidishaji vikali. VIKOMO VYA MFIDUO WA KAZI (OELS): TLV: 10 ppm kama TWA; 15 ppm kama STEL; (ngozi); A4 (ACGIH 2005). MAK: H Aina ya sarakani: 2; Aina inayoleta mabadiliko kwa seli za uzazi: 3B; (DFG 2004). |
NJIA ZA MFIDUO: Dutu hii huweza kufyonzwa ndani ya mwili kwa kuvuta pumzi, kupitia kwenye ngozi na kwa kumeza. HATARI ZA KUVUTA PUMZI: Ukolezi unaodhuru waweza kufikiwa polepole kutokana na uvukizi wa dutu hii ifikapo 20°C. Tazama Vidokezo. ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MFUPI: Dutu hii huweza kuathiri damukusababisha vidonda vya seli za damu (haemolysis). Tazama Vidokezo. Athari zinaweza kuchelewa. Mfiduo by ingestionhuweza kusababisha kifo. Uchunguzi wa kitibabu unahitajika. ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MREFU AU UNAORUDIWA: Dutu hii huweza kuathiri damu kusababisha upungufu wa chembechembe nyekundu za damu (chronic haemolytic anemia). Dutu hii huweza kuathiri jicho kusababisha mtoto wa jicho (development of cataract). Dutu hii ina uwezekano wa kusababisha kansa kwa binadamu. | ||
| TABIA ZA KIMAUMBILE | |||
|
Kiwango mchemko: 218°C Sublimation slowly at room temperature Kiwango myeyuko: 80°C Uzito wiani: 1.16 g/cm³ Umumunyifu katika maji, g/100 ml ifikapo 25°C: hakuna Kanieneo mvuke, Pa ifikapo 25°C: 11 Uzitowiani wa mvuke (hewa = 1): 4.42 |
Kiwango cha kumweka: 80°C c.c. Jotoridi la kujiwasha: 540°C Vikomo vya kilipukaji, % ujazo katika hewa: 0.9-5.9 Oktanoli/kizigeu mgawo cha maji kwa logi Pow: 3.3 | ||
| DATA YA MAZINGIRA | |||
|
Dutu hii ni sumu kali kwa viumbe viishivyo majini. Dutu hii inaweza kusababisha madhara yatakayoonekana baadaye katika mazingira ya maji.
| |||
| VIDOKEZO | |||
|
Baadhi ya watu wanaweza kuathiriwa zaidi na athari za nafthalini katika seli za damu
| |||
| MAELEZO YA ZIADA | |||
|
| |||
| |||
| © IPCS, CEC 2005 | |||