| ||||||||||||||
| ||||||||||||||
|
||||||||||||||
| AINA ZA HATARI / MFIDUO | MADHARA YA PAPO HAPO / DALILI | KINGA | HUDUMA YA KWANZA / UZIMAJI MOTO |
| MOTO |
Haiwaki. Hutoa moshi (au gesi) wenye kukereketa au wenye sumu ukiwa motoni.
|
|
Moto unapotokea katika eneo: vitenzi vyote vya kuzimia moto vinaruhusiwa.
|
| MLIPUKO |
|
|
Utokeapo moto: poza mapipa n.k. kwa kunyunyizia maji BILA (vilivyomo) kugusa maji.
|
| MFIDUO |
|
ZUIA MTAWANYIKO WA VUMBI! FUATA MASHARTI YA AFYA KIKAMILIFU!
|
KWA HALI YOYOTE MWONE DAKTARI!
|
| Kuvuta pumzi |
Kuumwa koo. Kuumwa kichwa. Kuchanganyikiwa. Udhaifu. Kukosa pumzi. Degedege. Kupoteza fahamu. Tazama Vidokezo.
|
Kinga kiambo ya utoaji moshi au kupumua.
|
Hewa safi, mapumziko. Pumulisha yaweza kuhitajika. Huduma ya kusaidia kupumua ya mdomo kwa mdomo hairuhusiwi. Tumia oksijeni inayotolewa na wataalamu. Mpeleke kwa matibabu.
|
| Ngozi |
YAWEZA KUFYONZWA! Wekundu. Maumivu. (Tazama Kuvuta pumzi).
|
Glavu za kinga. Mavazi ya kinga.
|
Vua nguo zilizosibikwa. Suuza ngozi kwa maji mengi au oga. Mpeleke kwa matibabu.
|
| Macho |
Wekundu. Maumivu.
|
Miwanivuli ya usalama, kingao cha uso, au kinga ya macho pamoja na kinga ya kupumulia.
|
Kwanza safisha macho vizuri kwa dakika chache (ondoa lenzi mboni kama inawezekana kuziondoa kwa urahisi), kisha mpeleke kwa daktari.
|
| Kumeza |
Mchomo. Kichefuchefu. Kutapika. Kuhara. (Tazama Kuvuta pumzi).
|
Usile, usinywe wala kuvuta sigara ukiwa kazini. Nawa mikono kabla ya kula.
|
Mtapishe (MTU MWENYE FAHAMU TU!). Vaa glavu za kinga unapotoa utapishi. Mpe tope chujio la mkaa ulioamilishwa katika maji anywe. Huduma ya kusaidia kupumua ya mdomo kwa mdomo hairuhusiwi. Tumia oksijeni inayotolewa na wataalamu. Mpeleke kwa daktari. Tazama Vidokezo.
|
| KUSAFISHA MWAGIKO | UFUNGASHAJI / UWEKAJI LEBO | |||||||
|
Ondoka katika eneo la hatari. Shauriana na mtaalam. Kinga ya ziada ya binafsi: nguo kamili za usalama pamoja na vifaa vya kupumulia vilivyo toshelevu. Uingizaji hewa. Zoa dutu iliyomwagika katika vyombo vinavyokalafatika. Kusanya salio kwa uangalifu, kisha peleka mahala pa usalama. Usiruhusu kemikali hii iingie katika mazingira.
|
Kisichoingiza hewa. Furushi madhubuti; weka furushi linaloweza kuvunjika katika chombo madhubuti kilichofungwa. Usisafirishe pamoja na vyakula au malisho. Kichafuzi cha maji/bahari. Ainisho ya EU Alama: T+, N R: 26/27/28-32-50/53 S: (1/2-)-7-28-29-45-60-61 Angalia: [A] Ainisho ya UN Ainisho ya UN ya Hatari: 6.1 Kikundi Ufungashaji cha UN: I | |||||||
| HATUA ZA HARAKA | UHIFADHI | |||||||
|
Kadi ya Dharura ya Usafiri: TEC(R) - 61GT5-I or 61GT5-I-Cy
|
Kinachotenganishwa na maunzi yasiokubaliana, vyakula na malisho. Kavu. Kilichofungwa vizuri. Weka katika chumba chenye uingizaji hewa mzuri. Hifadhi mahali pasipokuwa na unyevu au uchafu.
| |||||||
| ||||||||
| |||
| DATA MUHIMU | |||
|
HALI MAUMBILE; INAVYOONEKANA: FUWELE NYEUPE YENYE HARUFU KALI. HATARI ZA KIKEMIKALI: Dutu hii hutengana inapogusana na asidi, besi, amonia alkoholi, na inapokanzwa kuzalisha gesi zenye sumu pamoja na sianidi hidrojeni. Humenyuka pamoja na dioksidi kaboni au polepole pamoja na maji kusababisha sianidi hidrojeni. VIKOMO VYA MFIDUO WA KAZI (OELS): TLV haifahamiki. Ikichanganyika katika hewa nyevu huunda mazingira ya sianidi ya hidrojeni: TLV: (sianidi hidrojeni na baadhi ya chumvi za sianidi, kama CN) 4.7 ppm kama STEL; (kiwango cha juu); (ACGIH 2005). MAK: (as CN) (kiwango cha kunuswa) 2 mg/m³; Aina ya kiwango cha juu: II (1); Kuingia kupitia kwa ngozi (H); Kundi la waja wazito lililo hatarini: C; (DFG 2004). |
NJIA ZA MFIDUO: Dutu hii huweza kufyonzwa ndani ya mwili kwa kuvuta pumzi ya erosoli yake, kupitia kwenye ngozi na kwa kumeza. HATARI ZA KUVUTA PUMZI: Kikolezo cha chembechembeya dhuru yaweza kufikiwa haraka ikitawanywa. ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MFUPI: Dutu hii inakera kwa ukali macho ngozi na njia ya upumuaji. Dutu hii huweza kuathiri ubadilishaji hewa wa seli kusababisha degedege na kupoteza fahamu. Mfiduo huweza kusababisha kifo. Uchunguzi wa kitibabu unahitajika. Tazama Vidokezo. ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MREFU AU UNAORUDIWA: Dutu hii huweza kuathiri tezi thioridi. | ||
| TABIA ZA KIMAUMBILE | |||
|
Kiwango myeyuko: 146-147°C Uzito wiani: 2.84 g/cm³ Umumunyifu katika maji: mmenyuko kwa upole Kanieneo mvuke, Pa ifikapo 25.2°C: 130 Uzitowiani wa mvuke (hewa = 1): 1.54 |
|||
| DATA YA MAZINGIRA | |||
|
Dutu hii ni sumu kali kwa viumbe viishivyo majini.
| |||
| VIDOKEZO | |||
|
Matibabu mahsusi yanahitajika iwapo kuna uligaji kutokana na dutu hii; njia muafaka pamoja na maelekezo sharti yapatikane. Usichukue nguo za kazi nyumbani.
| |||
| MAELEZO YA ZIADA | |||
|
| |||
| |||
| © IPCS, CEC 2005 | |||