| ||||||||||||||
| ||||||||||||||
|
||||||||||||||
| AINA ZA HATARI / MFIDUO | MADHARA YA PAPO HAPO / DALILI | KINGA | HUDUMA YA KWANZA / UZIMAJI MOTO |
| MOTO |
Huungua. Tazama Vidokezo.
|
Usiwashe moto, usiwashe cheche, usivute sigara.
|
Mnyunyizio wa maji, povu linalokinza alkoholi, poda kavu, dioksidi kaboni.
|
| MLIPUKO |
Mvuke/hewa mahuluti inayolipuka huweza kufanyika inapovuka 58°C. (Tazama Vidokeso.)
|
Mfumo funge wa zaidi ya 58°C, uingizaji hewa, na vifaa vya umeme visivyolipuka. Tumia vifaa vya mkono visivyotoa cheche.
|
Utokeapo moto: poza mapipa, n.k. kwa kunyunyizia maji.
|
| MFIDUO |
|
|
|
| Kuvuta pumzi |
Kikohozi. Kuumwa koo.
|
Uingizaji hewa, mtambo wa kutolea nje, au kinga ya kupumulia.
|
Hewa safi, mapumziko.
|
| Ngozi |
Wekundu. Ngozi kavu. YAWEZA KUFYONZWA!
|
Glavu za kinga. Mavazi ya kinga.
|
Vua nguo zilizosibikwa. Suuza na kisha safisha ngozi kwa maji na sabuni.
|
| Macho |
Wekundu. Maumivu.
|
Miwanivuli ya usalama.
|
Kwanza safisha macho vizuri kwa dakika chache (ondoa lenzi mboni kama inawezekana kuziondoa kwa urahisi), kisha mpeleke kwa daktari.
|
| Kumeza |
|
Usile, usinywe wala kuvuta sigara ukiwa kazini.
|
Sukutua kinywa. Usimtapishe. Umpe maji mengi ya kunywa. Mpeleke kwa daktari.
|
| KUSAFISHA MWAGIKO | UFUNGASHAJI / UWEKAJI LEBO | |||||||
|
Ondoa vyanzo vyote vya moto. Kinga ya ziada ya binafsi: kipumulio chujio cha gesi na mivuke ya kikaboni. Funika dutu iliyomwagika kwa kifyonzi ajizi. Kusanya salio kwa uangalifu.
|
Ainisho ya EU Alama: Xi R: 36 S: (2-)-24/25 Ainisho ya UN Ainisho ya UN ya Hatari: 3 Kikundi Ufungashaji cha UN: III | |||||||
| HATUA ZA HARAKA | UHIFADHI | |||||||
|
Kadi ya Dharura ya Usafiri: TEC(R) - 30GF1-III Msimbo wa NFPA: H 1; F 2; R 0; |
Isodhurika kwa moto. Kinachotenganishwa na asidi, besi, amini na vioksidishaji.
| |||||||
| ||||||||
| |||
| DATA MUHIMU | |||
|
HALI MAUMBILE; INAVYOONEKANA: KIOEVU KISICHO RANGI CHENYE HARUFU TAMBULISHI. HATARI ZA KIKEMIKALI: Dutu hii hutengana inapokanzwa au inapochomwa au inapogusana na asidi, besi na amini, huzalisha asetoni, mesityl alcohol. Humenyuka kwa ukali sana pamoja na vioksidishaji kutoa gesi inayoweza kuwaka/kulipuka (hidrojeni - tazama ICSC 0001) VIKOMO VYA MFIDUO WA KAZI (OELS): TLV: 50 ppm kama TWA; (ACGIH 2005). MAK: 20 ppm, 96 mg/m³; Aina ya kiwango cha juu: I(2); kuingia kupitia kwa ngozi (H); Kundi la waja wazito lililo hatarini: IIc; (DFG 2004). |
NJIA ZA MFIDUO: Dutu hii huweza kufyonzwa ndani ya mwili kwa kuvuta pumzi ya mvuke wake, kupitia kwenye ngozi na kwa kumeza. HATARI ZA KUVUTA PUMZI: Mchanganyiko unaoweza kudhuru yaweza kutokea haiwezi au yaweza kufikia kwa upolekama dutu hii inavukiza kwa hewa yenye joto ya 20°C. ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MFUPI: Dutu hii inakera macho, ngozi na njia ya upumuaji. Kumeza kioevu hiki kunaweza kusababisha madhara kwenye mapafu kukifyonza na kunaweza kuleta kichomi kinachotokana na kemikali. Mfiduo juu ya OEL huweza kuleta kupungua kwa fahamu. ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MREFU AU UNAORUDIWA: Kioevu hukausha ngozi. | ||
| TABIA ZA KIMAUMBILE | |||
|
Kiwango mchemko: 169-171°C Kiwango myeyuko: -47°C Uzito wiani (maji = 1): 0.93 Umumunyifu katika maji: kuchanganyika Kanieneo mvuke, kPa ifikapo 20°C: 0.108 Uzitowiani wa mvuke (hewa = 1): 4.0 |
Uzito wiani wa mvuke/hewa mahuluti ifikapo 20°C (hewa = 1): 1.0048 Kiwango cha kumweka: 58°C c.c. Jotoridi la kujiwasha: 640°C Vikomo vya kilipukaji, % ujazo katika hewa: 1.8-6.9 Oktanoli/kizigeu mgawo cha maji kwa logi Pow: -0.14 to 1.03 (imekadiriwa) | ||
| DATA YA MAZINGIRA | |||
|
| |||
| VIDOKEZO | |||
|
Bidhaa ya kiufundi inaweza kuwa na hadi 5% ya asetoni (tazama ICSC0087) kusababisha kuwa na kiwango cha juu cha kuweza kuwaka. UN huainisha dutu kiteknikali kama 3 (ainisho ya UN ya hatari), II (kikundi ufungashaji cha UN).
| |||
| MAELEZO YA ZIADA | |||
|
| |||
| |||
| © IPCS, CEC 2005 | |||