| ||||||||||||||
| ||||||||||||||
|
||||||||||||||
| AINA ZA HATARI / MFIDUO | MADHARA YA PAPO HAPO / DALILI | KINGA | HUDUMA YA KWANZA / UZIMAJI MOTO |
| MOTO |
Huwaka. Hutoa moshi (au gesi) wenye kukereketa au wenye sumu ukiwa motoni.
|
Usiwashe moto.
|
Maji mengi.
|
| MLIPUKO |
Hatari ya moto na mlipuko.
|
USIACHE kikaathiriwa na msuguano au mshtuko.
|
Utokeapo moto: poza mapipa, n.k. kwa kunyunyizia maji. Zima moto ukiwa mahali pa usalama.
|
| MFIDUO |
|
ZUIA MTAWANYIKO WA VUMBI! FUATA MASHARTI YA AFYA KIKAMILIFU!
|
|
| Kuvuta pumzi |
(Tazama Kumeza).
|
Kinga kiambo ya utoaji moshi au kupumua.
|
Hewa safi, mapumziko. Mpeleke kwa matibabu.
|
| Ngozi |
YAWEZA KUFYONZWA! Wekundu. Ukwaru. Kubadilika kuwa njano. (Tazama Kuvuta pumzi).
|
Glavu za kinga. Mavazi ya kinga.
|
Vua nguo zilizosibikwa. Suuza ngozi kwa maji mengi au oga. Mpeleke kwa matibabu.
|
| Macho |
|
Miwanivuli ya usalama.
|
Kwanza safisha macho vizuri kwa dakika chache (ondoa lenzi mboni kama inawezekana kuziondoa kwa urahisi), kisha mpeleke kwa daktari.
|
| Kumeza |
Kichefuchefu. Kutapika. Mpapatiko. Kutokwa jasho. Kuzimia.
|
Usile, usinywe wala kuvuta sigara ukiwa kazini.
|
Kupumzika. Mpeleke kwa daktari.
|
| KUSAFISHA MWAGIKO | UFUNGASHAJI / UWEKAJI LEBO | |||||||
|
Ondoka katika eneo la hatari. Usiruhusu kukauka. Zoa dutu iliyomwagika katika vyombo. Pangusa salio katika mchanga au maunzi ajizi mengine kisha peleka mahala pa usalama. (Kinga ya ziada ya binafsi: nguo kamili za usalama pamoja na vifaa vya kupumulia vilivyo toshelevu).
|
Furushi madhubuti; weka furushi linaloweza kuvunjika katika chombo madhubuti kilichofungwa. Usisafirishe pamoja na vyakula au malisho. Kichafuzi cha maji/bahari. Ainisho ya EU Alama: T, N R: 23/24/25-33-50 S: (1/2-)-28-37-45-61 Ainisho ya UN Ainisho ya UN ya Hatari: 4.1 Jasara tanzu za UN: 6.1 Kikundi Ufungashaji cha UN: I | |||||||
| HATUA ZA HARAKA | UHIFADHI | |||||||
|
Kadi ya Dharura ya Usafiri: TEC(R) - 41GDT-I
|
Isodhurika kwa moto. Kinachotenganishwa na dutu zenye kuungua na za kunakisi, vyakula na malisho. Baridi.
| |||||||
| ||||||||
| |||
| DATA MUHIMU | |||
|
HALI MAUMBILE; INAVYOONEKANA: FUWELE MANJANO (tazama Vidokezo). HATARI KWA MWILI: Mlipuko wa vumbi huweza kutokea iwapo katika umbo la poda au punjepunje, vikichanganywa na hewa. HATARI ZA KIKEMIKALI: Huweza kutengana kwa mlipuko kutokana na mshtuko, msuguano, mtikiso. Huweza kulipuka wakati wa kukanza. Misombo isiyohimili mshtuko hutengenezwa kwa alkali, amonia na metali nyingi. Dutu hii hutengana inapokanzwa huzalisha gesi zenye sumu kama vile oksidi za nitrojeni. VIKOMO VYA MFIDUO WA KAZI (OELS): TLV haifahamiki |
NJIA ZA MFIDUO: Dutu hii huweza kufyonzwa ndani ya mwili kwa kuvuta pumzi, kupitia kwenye ngozi na kwa kumeza. HATARI ZA KUVUTA PUMZI: Uvukizi ifikapo 20°C ni kidogo; hata hivyo, ukolezi unaodhuru wa chembechembe zinazopeperuka hewani unaweza kufikiwa haraka. ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MFUPI: Dutu hii huweza kuathiri kimetaboliki, kusababisha joto la juu la mwili. Mfiduo huweza kusababisha kifo. ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MREFU AU UNAORUDIWA: Mgusano unaorudiwa au wa muda mrefu huweza kusababisha ugonjwa wa ngozi. Dutu hii huweza kuathiri mfumo wa neva wa pembeni. Dutu hii huweza kuathiri macho kutokuona kunakochelewa kutokea (cataract). | ||
| TABIA ZA KIMAUMBILE | |||
|
Kiwango mchemko: hujisablimisha Kiwango myeyuko: 112°C Uzito wiani (maji = 1): 1.68 Umumunyifu katika maji, g/100 ml ifikapo 54.5°C: 0.14 Uzitowiani wa mvuke (hewa = 1): 6.36 |
|||
| DATA YA MAZINGIRA | |||
|
Dutu hii inaweza kuwa na madhara kwa mazingira; tahadhari maalumu itolewe kwa viumbe hai vya majini.
| |||
| VIDOKEZO | |||
|
Tumia njia zote zilizopo kwa kupunguza jotoridi la mwili. Kwa sababu ya maumbile yake yakulipuka msombo hutumika pamoja na maji kama lahamu. UN 0076 hutumika kwa msombo mkavu. CAS 25550-58-7 hutumika kwa mchanganyiko ya isoma ya dinitrofenoli.
| |||
| MAELEZO YA ZIADA | |||
|
| |||
| |||
| © IPCS, CEC 2005 | |||