| |||||||||||||
| |||||||||||||
|
|||||||||||||
| AINA ZA HATARI / MFIDUO | MADHARA YA PAPO HAPO / DALILI | KINGA | HUDUMA YA KWANZA / UZIMAJI MOTO |
| MOTO |
Huwaka. Hutoa moshi (au gesi) wenye kukereketa au wenye sumu ukiwa motoni.
|
Usiwashe moto.
|
Poda, mnyunyizo wa maji, povu, dioksidi kaboni.
|
| MLIPUKO |
Mvuke/hewa mahuluti inayolipuka huweza kufanyika inapovuka 87°C.
|
Mfumo funge wa zaidi ya 87°C, uingizaji hewa, na vifaa vya umeme visivyolipuka.
|
Utokeapo moto: poza mapipa, n.k. kwa kunyunyizia maji.
|
| MFIDUO |
|
ZUIA UTOKAJI WA UKUNGU! FUATA MASHARTI YA AFYA KIKAMILIFU!
|
|
| Kuvuta pumzi |
Kuumwa kichwa. Kichefuchefu.
|
Uingizaji hewa, mtambo wa kutolea nje, au kinga ya kupumulia.
|
Hewa safi, mapumziko.
|
| Ngozi |
YAWEZA KUFYONZWA! Ngozi kavu.
|
Glavu za kinga. Mavazi ya kinga.
|
Vua nguo zilizosibikwa. Suuza na kisha safisha ngozi kwa maji na sabuni. Mpeleke kwa matibabu.
|
| Macho |
Wekundu. Kiwaa.
|
Miwani ya usalama.
|
Kwanza safisha macho vizuri kwa dakika chache (ondoa lenzi mboni kama inawezekana kuziondoa kwa urahisi), kisha mpeleke kwa daktari.
|
| Kumeza |
Kichefuchefu. Kutapika. Kusinzia.
|
Usile, usinywe wala kuvuta sigara ukiwa kazini.
|
Usimtapishe. Mpeleke kwa daktari.
|
| KUSAFISHA MWAGIKO | UFUNGASHAJI / UWEKAJI LEBO | |||||||
|
Uingizaji hewa. Kusanya kioevu kinachovuja na kilichomwagika katika vyombo vilivyozibwa kadri inavyowezekana. Fyonza kioevu kilichosalia katika mchanga au kifyonzi ajizi na kisha peleka mahala pa usalama. Special attention to avoid skin absorption. (Kinga ya ziada ya binafsi: kipumulio chujio cha gesi na mivuke ya kikaboni).
|
Ainisho ya EU Ainisho ya UN | |||||||
| HATUA ZA HARAKA | UHIFADHI | |||||||
|
Msimbo wa NFPA : H 1; F 1; R 0;
|
Kinachotenganishwa na vioksidishaji vikali. Baridi. Weka gizani. Weka katika chumba chenye uingizaji hewa mzuri.
| |||||||
| ||||||||
| |||
| DATA MUHIMU | |||
|
HALI MAUMBILE; INAVYOONEKANA: KIOEVU KIRISHAI KISICHO RANGI HATARI KWA MWILI: Mvuke huu ni mzito zaidi kuliko hewa na huweza kusafiri ardhini, uwakaji wa mbali unawezekana. HATARI ZA KIKEMIKALI: Dutu hii hutengana inapokanzwa au inapochomwa huzalisha mafusho yenye sumu kama vile oksidi za sulfuri. Humenyuka kwa ukali sana ikiwa na vioksidishaji vikali kama vile paklorati. VIKOMO VYA MFIDUO WA KAZI (OELS): TLV haifahamiki MAK: IIb (thamani ya MAK bado haijapatikana lakini hati kamili ipo) kuingia kupitia kwa ngozi (H); (DFG 2004). |
NJIA ZA MFIDUO: Dutu hii huweza kufyonzwa ndani ya mwili kwa kuvuta pumzi, kupitia kwenye ngozi na kwa kumeza. HATARI ZA KUVUTA PUMZI: Hakuna ashirio linaloweza kutolewa kuhusu kima ambacho ukolezi unaodhuru hufikiwa kutokana na uvukizi wa dutu hii ifikapo 20°C. ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MFUPI: Dutu hii inakera macho na ngozi. Mfiduo wa viwango vya juu ya dutu hii husababisha kupungua fahamu. Dutu hii yaweza kuongeza uwezo wa ngozi kufyonza ya kemikali nyinginezo (tazama Vidokezo). ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MREFU AU UNAORUDIWA: Mgusano unaorudiwa au wa muda mrefu huweza kusababisha ugonjwa wa ngozi. Dutu hii huweza kuathiri ini na damu, kusababisha kuharibika kwa utendaji na vidonda vya seli za damu. | ||
| TABIA ZA KIMAUMBILE | |||
|
Kiwango mchemko: 189°C Kiwango myeyuko: 18.5°C Uzito wiani (maji = 1): 1.1 Umumunyifu katika maji: kuchanganyika Kanieneo mvuke, Pa ifikapo 20°C: 59.4 Uzitowiani wa mvuke (hewa = 1): 2.7 |
Kiwango cha kumweka: 87°C c.c. Jotoridi la kujiwasha: 215°C Vikomo vya kilipukaji, % ujazo katika hewa: 2.6-42.0 Oktanoli/kizigeu mgawo cha maji kwa logi Pow: -1.35 (imekadiriwa) | ||
| DATA YA MAZINGIRA | |||
|
| |||
| VIDOKEZO | |||
|
Uangalifu mkubwa unatakiwa endapo DMSO ambayo ina sumu kali ipo; kwa sababu ya kuongezeka kwa uwezo wa ngozi wa kufyonza.
| |||
| MAELEZO YA ZIADA | |||
|
| |||
| |||
| © IPCS, CEC 2005 | |||