| |||||||||||||
| |||||||||||||
|
|||||||||||||
| AINA ZA HATARI / MFIDUO | MADHARA YA PAPO HAPO / DALILI | KINGA | HUDUMA YA KWANZA / UZIMAJI MOTO |
| MOTO |
Huwaka.
|
Usiwashe moto.
|
Mnyunyizio wa maji, povu, poda kavu, dioksidi kaboni.
|
| MLIPUKO |
Chembechembe zilizotawanyika hufanya mchanganyiko ulipukao hewani.
|
Zuia utuaji wa vumbi; mfumo funge, vifaa vya umeme na taa visivyolipuka kwa vumbi.
|
|
| MFIDUO |
|
ZUIA MTAWANYIKO WA VUMBI! EPUKA MGUSANO WOWOTE!
|
|
| Kuvuta pumzi |
Kikohozi. Kuumwa koo. Kufanyiza kisauti wakati wa kupumua.
|
Kinga kiambo ya utoaji moshi au kupumua.
|
Hewa safi, mapumziko. Mkao wa nusu wima. Mpeleke kwa matibabu.
|
| Ngozi |
Wekundu. Maumivu.
|
Glavu za kinga. Mavazi ya kinga.
|
Vua nguo zilizosibikwa. Suuza na kisha safisha ngozi kwa maji na sabuni. Mpeleke kwa matibabu.
|
| Macho |
Wekundu. Maumivu.
|
Miwanivuli ya usalama, au kinga ya macho pamoja na kinga ya kupumulia.
|
Kwanza safisha macho vizuri kwa dakika chache (ondoa lenzi mboni kama inawezekana kuziondoa kwa urahisi), kisha mpeleke kwa daktari.
|
| Kumeza |
Maumivu ya tumbo.
|
Usile, usinywe wala kuvuta sigara ukiwa kazini.
|
Sukutua kinywa. Usimtapishe. Umpe maji mengi ya kunywa. Mpeleke kwa daktari.
|
| KUSAFISHA MWAGIKO | UFUNGASHAJI / UWEKAJI LEBO | |||||||
|
Zoa dutu iliyomwagiga katika vyombo vilivyofunikwa; endapo inafaa, loanisha kwanza ili kuzuia vumbi. Kusanya salio kwa uangalifu, kisha peleka mahala pa usalama. Kinga ya ziada ya binafsi: vazi linalokinga kemikali linalojumuisha kifaa binafsi cha kupumulia.
|
Usisafirishe pamoja na vyakula au malisho. Ainisho ya EU Alama: Xn R: 22-37/38-41-42/43 S: (2-)-23-24/25-26-37/39-46 Ainisho ya UN | |||||||
| HATUA ZA HARAKA | UHIFADHI | |||||||
|
Msimbo wa NFPA: H 3; F 1; R 0;
|
Kinachotenganishwa na dutu zenye kuungua na za kunakisi, vioksidishaji vikali, besi kali, asidi kali, vyakula na malisho. Tazama Hatari za Kikemikali. Uingizaji hewa kwenye sakafu. Kavu. Kilichofungwa vizuri.
| |||||||
| ||||||||
| |||
| DATA MUHIMU | |||
|
HALI MAUMBILE; INAVYOONEKANA: FUWELE ING'ARAYO NYEUPE YENYE HARUFU TAMBULISHI. HATARI KWA MWILI: Mlipuko wa vumbi huweza kutokea iwapo katika umbo la poda au punjepunje, vikichanganywa na hewa. HATARI ZA KIKEMIKALI: Dutu hii hutengana inapogusana na maji ya moto huzalisha asidi ya ftaliki. Humenyuka ikiwa na vioksidishaji vikali, asidi kali, besi kali na kinakisishaji. Kwa kuichoma humenyuka kwa ukali pamoja na oksidi ya shaba au nitriti sodi kusababisha athari ya mlipuko. Hushambulia metali nyingi iwapo kuna maji. VIKOMO VYA MFIDUO WA KAZI (OELS): TLV: 1 ppm kama TWA; SEN; A4 (haijaainishwa kama kasinojeni kwa binadamu); (ACGIH 2003). MAK: IIb (thamani ya MAK bado haijapatikana lakini hati kamili ipo); uhisishaji wa koromeo la hewa (Sa); (DFG 2002). |
NJIA ZA MFIDUO: Dutu hii huweza kufyonzwa ndani ya mwili kwa kuvuta pumzi ya erosoli yake na kwa kumeza. HATARI ZA KUVUTA PUMZI: Kikolezo cha chembechembe zilizo hewani yaweza kufikiwa haraka ikitawanywa hasa kama poda. ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MFUPI: Dutu hii inakera kwa ukali irritating to macho, ngozi na njia ya upumuaji. ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MREFU AU UNAORUDIWA: Mgusano unaorudiwa au wa muda mrefu huweza kuhisisha ngozi. Kuvuta hewa kwa kurudia au muda mrefu huweza kusababisha pumu (ona Vidokezo). | ||
| TABIA ZA KIMAUMBILE | |||
|
Kiwango mchemko: 284°C (usablimishaji) Kiwango myeyuko: 131°C Uzito wiani: 1.53 g/cm³ Umumunyifu katika maji: mmenyuko kwa polepole Kanieneo mvuke, Pa ifikapo 20°C: <0.3 Uzitowiani wa mvuke (hewa = 1): 5.1 |
Kiwango cha kumweka: 152°C c.c. Jotoridi la kujiwasha: 570°C Vikomo vya kilipukaji, % ujazo katika hewa: 1.7-10.4 Oktanoli/kizigeu mgawo cha maji kwa logi Pow: 1.6 | ||
| DATA YA MAZINGIRA | |||
|
| |||
| VIDOKEZO | |||
|
Dutu hii inaweza kusafirishwa ikiwa katika hali ya kuyeyuka. Aghalabu dalili za pumu hazijitokezi mpaka baada ya masaa kadhaa kupita, nazo hushitadi kwa kazi za sulubu. Kwa hiyo mapumziko na uchunguzi wa kitibabu ni muhimu. Mtu yeyote aliyeonyesha dalili za pumu kutokana na dutu hii kamwe asigusane na dutu hiyo tena. Kwa vitu vyenye zaidi ya 0.05% ya anhidridi maleiki (maleic anhydride) namba ya UN ni 2214, daraja la 8 la hatari, kundi la III la kufungashwa na kadi ya Dharura ya kusafirishia ni TEC (R)-80S2214. Usichukue nguo za kazi nyumbani.
| |||
| MAELEZO YA ZIADA | |||
|
| |||
| |||
| © IPCS, CEC 2005 | |||