| ||||||||||||||
| ||||||||||||||
|
||||||||||||||
| AINA ZA HATARI / MFIDUO | MADHARA YA PAPO HAPO / DALILI | KINGA | HUDUMA YA KWANZA / UZIMAJI MOTO |
| MOTO |
Huungua sana. Hutoa moshi (au gesi) wenye kukereketa au wenye sumu ukiwa motoni.
|
Usiwashe moto, usiwashe cheche, usivute sigara. Usigusishe na unyevuunyevu, asidi, halojeni na dutu nyingine nyingi.
|
Poda maalum, mchanga mkavu, USITUMIE kitenzi kingine. USITUMIE maji.
|
| MLIPUKO |
Chembechembe zilizotawanyika hufanya mchanganyiko ulipukao hewani.
|
USIACHE kikaathiriwa na msuguano au mshtuko. Zuia mlimbiko wa chaji za umemetuamo (k.m. kwa kutuliza).
|
|
| MFIDUO |
|
ZUIA MTAWANYIKO WA VUMBI!
|
|
| Kuvuta pumzi |
Kikohozi. Kupumua kwa shida. Kuumwa kichwa. Mazimbwezimbwe. Udhaifu. Homa au kuongezeka joto la mwili.
|
|
|
| Ngozi |
|
|
|
| Macho |
Wekundu. Maumivu.
|
Miwanivuli ya usalama.
|
|
| Kumeza |
Maumivu ya tumbo. Kuhara.
|
Usile, usinywe wala kuvuta sigara ukiwa kazini.
|
Sukutua kinywa. Mpeleke kwa daktari.
|
| KUSAFISHA MWAGIKO | UFUNGASHAJI / UWEKAJI LEBO | |||||||
|
Usielekeze kwenye mfereji wa maji machafu. Zoa dutu iliyomwagika katika vyombo. Kusanya salio kwa uangalifu, kisha peleka mahala pa usalama. (Kinga ya ziada ya binafsi: kipumulio chujio P2 cha chembe zinazodhuru).
|
Kisichoingiza hewa. Ainisho ya EU Alama: F R: 15-17 S: (2-)-7/8-43 Ainisho ya UN Ainisho ya UN ya Hatari: 4.3 Jasara tanzu za UN: 4.2 Kikundi Ufungashaji cha UN: ll | |||||||
| HATUA ZA HARAKA | UHIFADHI | |||||||
|
Kadi ya Dharura ya Usafiri: TEC(R) - 43GWS-II+III Msimbo wa NFPA : H 0; F 1; R 2; |
Isodhurika kwa moto. Kinachotenganishwa na vioksidishaji vikali, asidi. Kavu.
| |||||||
| ||||||||
| |||
| DATA MUHIMU | |||
|
HALI MAUMBILE; INAVYOONEKANA: PODA KIJIVU HATARI KWA MWILI: Mlipuko wa vumbi huweza kutokea iwapo katika umbo la poda au punjepunje, vikichanganywa na hewa. HATARI ZA KIKEMIKALI: Dutu hii huweza kuwaka papo hapo inapogusana na hewa au unyevuunyevu kutoa mafusho yenye sumu. Humenyuka kwa ukali sana ikiwa na vioksidishaji vikali. Humenyuka kwa ukali sana pamoja na misombo mingi kusababisha athari ya moto na mlipuko. Humenyuka pamoja na asidi na maji kutoa gesi yanayoweza kuwaka (hidrojeni tazama ICSC0001), kusababisha athari ya moto na mlipuko. VIKOMO VYA MFIDUO WA KAZI (OELS): TLV haifahamiki MAK haifahamiki |
NJIA ZA MFIDUO: Dutu hii huweza kufyonzwa ndani ya mwili kwa kuvuta pumzi. HATARI ZA KUVUTA PUMZI: Uvukizi ifikapo 20°C ni kidogo; hata hivyo, ukolezi unaodhuru wa chembechembe zinazopeperuka hewani unaweza kufikiwa haraka. ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MFUPI: Kuvuta hewa yenye mafusho kunaweza kusababisha homa ya metali. | ||
| TABIA ZA KIMAUMBILE | |||
|
Kiwango mchemko: 1100°C Kiwango myeyuko: 651°C Uzito wiani: 1.7 g/cm³ Umumunyifu katika maji: hakuna |
Jotoridi la kujiwasha: 473°C Vikomo vya kilipukaji, % ujazo katika hewa: tazama Vidokezo | ||
| DATA YA MAZINGIRA | |||
|
| |||
| VIDOKEZO | |||
|
Huwaka kwa mwale mkali sana. Ili kuzuia macho yasiumie usiangalie mwale wa magnesi bila kinga. Humenyuka kwa nguvu na vitenzi vya kuzimia moto kama vile maji, dioksidi kaboni na poda. Vikomo vya kilipukaji, % ujazo katika hewa: (LEL) 0.03 kg/m³.
| |||
| MAELEZO YA ZIADA | |||
|
| |||
| |||
| © IPCS, CEC 2005 | |||