| ||||||||||||||
| ||||||||||||||
|
||||||||||||||
| AINA ZA HATARI / MFIDUO | MADHARA YA PAPO HAPO / DALILI | KINGA | HUDUMA YA KWANZA / UZIMAJI MOTO |
| MOTO |
Haiwaki. Mimenyuko mingi yaweza kusababisha moto au kulipuka.
|
|
Moto unapotokea katika eneo: vitenzi vyote vya kuzimia moto vinaruhusiwa.
|
| MLIPUKO |
|
|
Utokeapo moto: poza silinda kwa kunyunyizia maji BILA (vilivyomo) kugusa maji. Zima moto ukiwa mahali pa usalama.
|
| MFIDUO |
|
EPUKA MGUSANO WOWOTE!
|
KWA HALI YOYOTE MWONE DAKTARI!
|
| Kuvuta pumzi |
Mchomo. Kikohozi. Kizunguzungu. Kuumwa kichwa. Kupumua kwa shida. Kichefuchefu. Kukosa pumzi. Kuumwa koo. Kutapika. Dalili zinaweza kuchelewa (tazama Vidokezo).
|
Uingizaji hewa, mtambo wa kutolea nje, au kinga ya kupumulia.
|
Hewa safi, mapumziko. Mkao wa nusu wima. Mpeleke kwa matibabu.
|
| Ngozi |
YAWEZA KUFYONZWA! Wekundu. Maumivu. Mibabuko ya ngozinzito. Malengelenge. (Tazama Kuvuta pumzi).
|
Glavu za kinga. Mavazi ya kinga.
|
Vua nguo zilizosibikwa. Suuza ngozi kwa maji mengi au oga. Mpeleke kwa matibabu.
|
| Macho |
Wekundu. Maumivu. Kuungua kunakopenya sana.
|
Kingao cha uso, au kinga ya macho pamoja na kinga ya kupumulia.
|
Kwanza safisha macho vizuri kwa dakika chache (ondoa lenzi mboni kama inawezekana kuziondoa kwa urahisi), kisha mpeleke kwa daktari.
|
| Kumeza |
Maumivu ya tumbo. Mchomo. Kuhara. Kichefuchefu. Kutapika. Udhaifu. Zirai.
|
Usile, usinywe wala kuvuta sigara ukiwa kazini. Nawa mikono kabla ya kula.
|
Sukutua kinywa. Usimtapishe. Mpeleke kwa daktari.
|
| KUSAFISHA MWAGIKO | UFUNGASHAJI / UWEKAJI LEBO | |||||||
|
Ondoka katika eneo la hatari. Shauriana na mtaalam. Uingizaji hewa. Ondoa mvuke kwa mnyunyuzio mwembamba wa maji. Vazi linalokinga kemikali linaloruhusu gesi linalojumuisha kifaa binafsi cha kupumulia.
|
Usisafirishe pamoja na vyakula au malisho. Ainisho ya EU Alama: T+, C R: 26/27/28-35 S: (1/2-)-7/9-26-36/37/39-45 Ainisho ya UN Ainisho ya UN ya Hatari: 8 Jasara tanzu za UN: 6.1 | |||||||
| HATUA ZA HARAKA | UHIFADHI | |||||||
|
Kadi ya Dharura ya Usafiri: TEC(R) - 80S1052 au 80GCT1-I Msimbo wa NFPA : H 3; F 0; R 2; |
Isodhurika kwa moto. Kinachotenganishwa na vyakula na malisho. Tazama Hatari za Kikemikali. Baridi. Weka katika chumba chenye uingizaji hewa mzuri.
| |||||||
| ||||||||
| |||
| DATA MUHIMU | |||
|
HALI MAUMBILE; INAVYOONEKANA: GESI ISO RANGI AU KIOEVU KISICHO RANGI, KIFUKACHO, CHENYE HARUFU KALI. HATARI ZA KIKEMIKALI: Dutu hii ni asidi kali, humenyuka vikali ikiwa na besi na husababisha ulikaji. Humenyuka kwa ukali sana pamoja na misombo mingi kusababisha athari ya moto na mlipuko. Hushambulia metali, kioo, aina fulani za plastiki, mpira na mipako. VIKOMO VYA MFIDUO WA KAZI (OELS): TLV: (as F) 0.5 ppm kama TWA, 2 ppm (kiwango cha juu); BEI imetolewa; (ACGIH 2005). MAK: 2 ppm, 1.7 mg/m³; Aina ya kiwango cha juu: I(2); Kundi la waja wazito lililo hatarini: C; MAK: BAT 7 mg/g creatinine; (DFG 2005). |
NJIA ZA MFIDUO: Dutu hii huweza kufyonzwa ndani ya mwili kwa kuvuta pumzi, kupitia kwenye ngozi na kwa kumeza. HATARI ZA KUVUTA PUMZI: Ukolezi unaodhuru wa gesi hii hewani utafikiwa kwa haraka sana isipodhibitiwa. ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MFUPI: Dutu hii husababisha ulikaji kwa macho, ngozi na njia ya upumuaji. Kuvuta pumzi yenye gesi au mvuke kunaweza kusababisha uvimbe wa mapafu (tazama Vidokezo). Dutu hii yaweza kudukiza upungufu na kalsiamu ya damu (hypocalcemia). Mfiduo zaidi ya OEL huweza kusababisha kifo. Athari zinaweza kuchelewa. Uchunguzi wa kitibabu unahitajika. ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MREFU AU UNAORUDIWA: Dutu hii huweza kusababisha mabadiliko kwa mifupa na meno kwa sababu ya florini (fluorosis). | ||
| TABIA ZA KIMAUMBILE | |||
|
Kiwango mchemko: 20°C Kiwango myeyuko: -83°C Uzito wiani (maji = 1): 1.0 kioevu ifikapo 4°C Umumunyifu katika maji: vizuri sana Kanieneo mvuke, kPa ifikapo 25°C: 122 Uzitowiani wa mvuke (hewa = 1): 0.7 |
|||
| DATA YA MAZINGIRA | |||
|
| |||
| VIDOKEZO | |||
|
Kikomo thamani cha mfiduo matumizi ya kazi kisivukwe wakati wowote wa mfiduo amilifu. Dalili za uvimbe wa mapafu aghalabu hazijitokezi mpaka baada ya masaa kadhaa kupita, nazo hushitadi kwa kazi za sulubu. Hivyo mapumziko na uchunguzi wa kitibabu ni muhimu. Matumizi ajilani ya mnyunyuzio mwafaka unaotolewa na daktari au mtu aliyeidhinishwa naye yanahitajika. Pindua silinda ivujayo ili mvujio uwe juu kuzuia gesi isitoke katika hali ya uoevu. Kutegemeana na kiasi cha mfiduo, upimaji wa kitibabu wa mara kwa mara unahitajika. Namba ya muungano wa mataifa (UN) kwa hidrojeni floraidi ya mmumunyo wa majimaji: 1790, ainisho ya hatari 8, jasara tanzu za UN 6.1, kikundi ufungashaji I (>60%).
| |||
| MAELEZO YA ZIADA | |||
|
| |||
| |||
| © IPCS, CEC 2005 | |||