| ||||||||||||||
| ||||||||||||||
|
||||||||||||||
| AINA ZA HATARI / MFIDUO | MADHARA YA PAPO HAPO / DALILI | KINGA | HUDUMA YA KWANZA / UZIMAJI MOTO |
| MOTO |
Haiwaki.
|
|
Moto unapotokea katika eneo: vitenzi vyote vya kuzimia moto vinaruhusiwa.
|
| MLIPUKO |
Tazama Vidokezo.
|
|
Utokeapo moto: poza mapipa, n.k. kwa kunyunyizia maji.
|
| MFIDUO |
|
FUATA MASHARTI YA AFYA KIKAMILIFU!
|
KWA HALI YOYOTE MWONE DAKTARI!
|
| Kuvuta pumzi |
Mchomo. Kikohozi. Kupumua kwa shida. Kukosa pumzi. Kuumwa koo.
|
Uingizaji hewa, mtambo wa kutolea nje, au kinga ya kupumulia. Kilichofungwa viwekeo vizuri.
|
Hewa safi, mapumziko. Pumulisha iwapo imeelezwa. Mpeleke kwa matibabu.
|
| Ngozi |
Inababua. Wekundu. Mibabuko ya ngozi nzito. Maumivu. Malengelenge.
|
Glavu za kinga. Mavazi ya kinga.
|
Vua nguo zilizosibikwa. Suuza ngozi kwa maji mengi au oga. Mpeleke kwa matibabu.
|
| Macho |
Inababua. Wekundu. Maumivu. Kiwaa. Kuungua kunakopenya sana.
|
Kingao cha uso, au kinga ya macho pamoja na kinga ya kupumulia.
|
Kwanza safisha macho vizuri kwa dakika chache (ondoa lenzi mboni kama inawezekana kuziondoa kwa urahisi), kisha mpeleke kwa daktari.
|
| Kumeza |
Inababua. Msokoto wa tumbo. Maumivu ya tumbo. Kuumwa koo. Kutapika. (Tazama Kuvuta pumzi).
|
Usile, usinywe wala kuvuta sigara ukiwa kazini.
|
Sukutua kinywa. Usimtapishe. Umpe maji mengi ya kunywa. Mpeleke kwa daktari.
|
| KUSAFISHA MWAGIKO | UFUNGASHAJI / UWEKAJI LEBO | |||||||
|
Ondoka katika eneo la hatari. Shauriana na mtaalam endapo kiasi kikubwa kimemwagika. Uingizaji hewa. Katisha kioevu kilichomwagika kwa uangalifu kwa asidi iliyozimuliwa, kama vile asidi sulfuriki iliyozimuliwa. Osha salio kwa maji mengi. Usiruhusu kemikali hii iingie katika mazingira. (Kinga ya ziada ya binafsi: nguo kamili za usalama pamoja na vifaa vya kupumulia vilivyo toshelevu).
|
Furushi madhubuti; weka furushi linaloweza kuvunjika katika chombo madhubuti kilichofungwa. Ainisho ya EU Alama: C, N R: 34-50 S: (1/2-)-26-36/37/39-45-61 Angalia: [B] Ainisho ya UN Ainisho ya UN ya Hatari: 8 Kikundi Ufungashaji cha UN: III | |||||||
| HATUA ZA HARAKA | UHIFADHI | |||||||
|
Kadi ya Dharura ya Usafiri: TEC(R) - 80S2672 Msimbo wa NFPA : H 3; F 1; R 0; |
Kinachotenganishwa na vyakula na malisho (tazama Hatari za Kikemikali). Baridi. Kilichofungwa vizuri. Weka katika chumba chenye uingizaji hewa mzuri.
| |||||||
| ||||||||
| |||
| DATA MUHIMU | |||
|
HALI MAUMBILE; INAVYOONEKANA: MMUMUNYO UVUKAO SANA WA AMMONIA WA MAJI, USIO RANGI, WENYE HARUFU KALI. HATARI ZA KIKEMIKALI: Humenyuka pamoja na metali nzito nyingi na chumvi zake kufanyiza misombo lipukaji. Hushambulia metali nyingi na kutoa gesi inayoweza kuwaka/lipukaji (Hidrojeni - tazama ICSC 0001). Mmumunyo huu katika maji ni besi kali, inamenyuka kwa ukali sana na asidi. VIKOMO VYA MFIDUO WA KAZI (OELS): TLV: (gesi NH_3) 25 ppm kama TWA; 40 ppm kama STEL; (ACGIH 2004). MAK: 20 ppm, 14 mg/m³; Aina ya kiwango cha juu: I(2); Kundi la waja wazito lililo hatarini: C; (DFG 2004). |
NJIA ZA MFIDUO: Dutu hii huweza kufyonzwa ndani ya mwili kwa kuvuta pumzi ya mvuke wake au aerosol na kwa kumeza. HATARI ZA KUVUTA PUMZI: Ukolezi unaodhuru unaweza kufikiwa haraka sana kutokana na uvukizi wa dutu hii ifikapo 20°C. ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MFUPI: Dutu hii husababisha ulikaji kwa macho, ngozi na njia ya upumuaji. Husababisha ubabuzi inapomezwa. Kuvuta pumzi yenye kiwango kikubwa cha mvuke kunaweza kusababisha kuvimba wa koo na mibabuko katika njia ya kupumulia, na kichomi. Athari zinaweza kuchelewa. ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MREFU AU UNAORUDIWA: Mapafu huathirika na mfiduo unaorudiwa au wa muda mrefu kwa mvuke au erosoli. | ||
| TABIA ZA KIMAUMBILE | |||
|
Kiwango mchemko: (25%) 38°C Kiwango myeyuko: (25%) -58°C Uzito wiani (maji = 1): (25%) 0.9 Umumunyifu katika maji: kuchanganyika Kanieneo mvuke, kPa ifikapo 20°C: (25%) 48 Uzitowiani wa mvuke (hewa = 1): 0.6-1.2 |
|||
| DATA YA MAZINGIRA | |||
|
Dutu hii ni sumu kali kwa viumbe viishivyo majini.
| |||
| VIDOKEZO | |||
|
Katika hali fulani mvuke wa amonia unaweza kuwaka na kulipuka. Ufahamu kuwa gesi ya amonia yaweza kufuka kutoka kwenye mmumunyo wa amonia. Kutegemeana na kiasi cha mfiduo, upimaji wa kitibabu wa mara kwa mara unahitajika. Usijaze chupa na dutu hii hadi juu, mimumunyo mikali yaweza kusababisha msukumo. Fungua kwa uangalifu. Nambari nyingine za UN ni UN 1005 Amonia, anhidrasi kimiminika au mmumunyo wa amonia, uzito wiani wa pungufu ya 0.880 katika 15°C kwenye maji, ikiwa na amonia zaidi ya 50%; UN 2073 Amonia, 35-50%. Pia shauriana na ICSC #0414 Amonia.
| |||
| MAELEZO YA ZIADA | |||
|
| |||
| |||
| © IPCS, CEC 2005 | |||