| ||||||||||||||
| ||||||||||||||
|
||||||||||||||
| AINA ZA HATARI / MFIDUO | MADHARA YA PAPO HAPO / DALILI | KINGA | HUDUMA YA KWANZA / UZIMAJI MOTO |
| MOTO |
Haiwaki lakini huongeza mwako wa dutu nyingine. Hutoa moshi (au gesi) wenye kukereketa au wenye sumu ukiwa motoni.
|
Usiwashe moto, usiwashe cheche, usivute sigara.
|
Moto unapotokea katika eneo: vitenzi vyote vya kuzimia moto vinaruhusiwa.
|
| MLIPUKO |
Hatari ya moto na mlipuko: Tazama Hatari za Kikemikali.
|
Mfumo funge, uingizaji hewa, na vifaa vya umeme na taa visivyolipuka.
|
Utokeapo moto: poza silinda kwa kunyunyizia maji. Zima moto ukiwa mahali pa usalama.
|
| MFIDUO |
|
EPUKA MFIDUO KWA WANAWAKE (WAJAWAZITO)!
|
|
| Kuvuta pumzi |
Kusikia raha (nishai). Kusinzia. Kupoteza fahamu.
|
Uingizaji hewa. Kinga kiambo ya utoaji moshi au kupumua.
|
Hewa safi, mapumziko. Mpeleke kwa matibabu.
|
| Ngozi |
INAPOGUSANA NA KIOEVU: JAMIDI.
|
Glavu za kuhami baridi.
|
UPATAPO JAMIDI: suuza kwa maji mengi, USIVUE nguo. Mpeleke kwa matibabu.
|
| Macho |
INAPOGUSANA NA KIOEVU: JAMIDI.
|
Miwanivuli ya usalama, au kinga ya macho pamoja na kinga ya kupumulia.
|
Kwanza safisha macho vizuri kwa dakika chache (ondoa lenzi mboni kama inawezekana kuziondoa kwa urahisi), kisha mpeleke kwa daktari.
|
| Kumeza |
|
Usile, usinywe wala kuvuta sigara ukiwa kazini.
|
|
| KUSAFISHA MWAGIKO | UFUNGASHAJI / UWEKAJI LEBO | |||||||
|
Ondoka katika eneo la hatari. Shauriana na mtaalam. Uingizaji hewa. Ikiwa ni kioevu: usifyonze katika vumbi la mbao au vifyonzi vinginevyo viwakavyo. KAMWE usielekeze nyiri ya maji juu ya kioevu. Kinga ya ziada ya binafsi: vifaa vya kupumulia vilivyo toshelevu.
|
Ainisho ya EU Ainisho ya UN Ainisho ya UN ya Hatari: 2.2 Jasara tanzu za UN: 5.1 | |||||||
| HATUA ZA HARAKA | UHIFADHI | |||||||
|
Kadi ya Dharura ya Usafiri: TEC(R) - 20S1070
|
Isodhurika kwa moto iwapo ndani ya jengo. Kinachotenganishwa na maunzi yasiokubaliana. Tazama Hatari za Kikemikali. Baridi.
| |||||||
| ||||||||
| |||
| DATA MUHIMU | |||
|
HALI MAUMBILE; INAVYOONEKANA: GESI OEVU ILIYOBANWA ISO RANGI YENYE HARUFU TAMBULISHI. HATARI KWA MWILI: Gesi hii ni nzito kuliko hewa na huweza kujilimbikiza katika eneo ambalo dari liko chinichini na kusababisha upungufu wa oksijeni. HATARI ZA KIKEMIKALI: Humenyuka kwa ukali sana pamoja na anhidridi sulfurasi, amofasi boroni, fosfini, etha, alumini, hidrazini, fenili-lithiamu na kabaidi tangisteni kusababisha athari ya moto na mlipuko. Ikizi 300°C gesi hii ni kioksidishaji kikali na yaweza kutengeneza mchanganyiko ulipukao kukiwepo amonia, monoksidi kaboni, salfidi hidrojeni, mafuta, grisi na fueli. VIKOMO VYA MFIDUO WA KAZI (OELS): TLV: 50 ppm kama TWA; A4; (ACGIH 2004). MAK: 100 ppm, 180 mg/m³; Aina ya kiwango cha juu: II(2); Kundi la waja wazito lililo hatarini: D; (DFG 2004). |
NJIA ZA MFIDUO: Dutu hii huweza kufyonzwa ndani ya mwili kwa kuvuta pumzi. HATARI ZA KUVUTA PUMZI: Ukolezi unaodhuru wa gesi hii hewani utafikiwa kwa haraka sana isipodhibitiwa. ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MFUPI: Kioevu hiki huweza kusababisha jamidi. Dutu hii huweza kuathiri mfumo mkuu wa neva kusababisha kupungua kwa fahamu. ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MREFU AU UNAORUDIWA: Dutu hii huweza kuathiri uboho na mfumo wa neva wa pembeni. Inaweza kusababisha kusumisha kwa uzazi na kukua kwa binadamu. | ||
| TABIA ZA KIMAUMBILE | |||
|
Kiwango mchemko: -88.5°C Kiwango myeyuko: -90.8°C Uzito wiani (maji = 1): 1.23 ifikapo -89°C Umumunyifu katika maji, g/100 ml ifikapo 15°C: 0.15 Kanieneo mvuke, kPa ifikapo 20°C: 5150 Uzitowiani wa mvuke (hewa = 1): 1.53 |
Oktanoli/kizigeu mgawo cha maji kwa logi Pow: 0.35 | ||
| DATA YA MAZINGIRA | |||
|
| |||
| VIDOKEZO | |||
|
Pindua silinda ivujayo ili mvujio uwe juu kuzuia gesi isitoke katika hali ya uoevu. Nambari nyingine ya UN: 2201 Kioevu baridi mno.
| |||
| MAELEZO YA ZIADA | |||
|
| |||
| |||
| © IPCS, CEC 2005 | |||