| ||||||||||||||
| ||||||||||||||
|
||||||||||||||
| AINA ZA HATARI / MFIDUO | MADHARA YA PAPO HAPO / DALILI | KINGA | HUDUMA YA KWANZA / UZIMAJI MOTO |
| MOTO |
Haiwaki. Hutoa moshi (au gesi) wenye kukereketa au wenye sumu ukiwa motoni.
|
|
Moto unapotokea katika eneo: vitenzi vyote vya kuzimia moto vinaruhusiwa.
|
| MLIPUKO |
|
|
|
| MFIDUO |
|
EPUKA MGUSANO WOWOTE! ZUIA MTAWANYIKO WA VUMBI! EPUKA MFIDUO KWA WANAWAKE (WAJAWAZITO)! EPUKA MFIDUO KWA VIJANA NA WATOTO!
|
|
| Kuvuta pumzi |
Kikohozi. Kuumwa kichwa. Kichefuchefu.
|
Kinga kiambo ya utoaji moshi au kupumua.
|
Hewa safi, mapumziko.
|
| Ngozi |
Ona ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MREFU AU UNAORUDIWA.
|
Glavu za kinga. Mavazi ya kinga.
|
Suuza na kisha safisha ngozi kwa maji na sabuni.
|
| Macho |
Wekundu.
|
Miwanivuli ya usalama, au kinga ya macho pamoja na kinga ya kupumulia iwapo poda.
|
Kwanza safisha macho vizuri kwa dakika chache (ondoa lenzi mboni kama inawezekana kuziondoa kwa urahisi), kisha mpeleke kwa daktari.
|
| Kumeza |
Maumivu ya tumbo. Kichefuchefu. Kutapika.
|
Usile, usinywe wala kuvuta sigara ukiwa kazini.
|
Sukutua kinywa. Umpe maji mengi ya kunywa.
|
| KUSAFISHA MWAGIKO | UFUNGASHAJI / UWEKAJI LEBO | |||||||
|
Vuta kiombwe maunzi yaliyomwagika au zoa dutu iliyomwagiga katika vyombo; endapo inafaa, loanisha kwanza ili kuzuia vumbi. Kusanya salio kwa uangalifu, kisha peleka mahala pa usalama. Usiruhusu kemikali hii iingie katika mazingira. (Kinga ya ziada ya binafsi: kipumulio chujio P3 cha chembe zenye sumu).
|
Furushi madhubuti; weka furushi linaloweza kuvunjika katika chombo madhubuti kilichofungwa. Kichafuzi cha maji/bahari. Ainisho ya EU Alama: T, N R: 61-33-40-50/53-62 S: 53-45-60-61 Ainisho ya UN Ainisho ya UN ya Hatari: 6.1 Kikundi Ufungashaji cha UN: III | |||||||
| HATUA ZA HARAKA | UHIFADHI | |||||||
|
Kadi ya Dharura ya Usafiri: TEC(R) - 61GT5-III
|
Kinachotenganishwa na vioksidishaji vikali.
| |||||||
| ||||||||
| |||
| DATA MUHIMU | |||
|
HALI MAUMBILE; INAVYOONEKANA: PODA FUWELE MANJANO HADI RANGI YA MACHUNGWA HATARI ZA KIKEMIKALI: Dutu hii hutengana inapokanzwa huzalisha mafusho yenye sumu pamoja na oksidi ya risasi. Humenyuka ikiwa na vioksidishaji vikali kama vile peroksidi hidrojeni. Humenyuka pamoja na alumini dinitronaftalini, feri(III) heksasianoferrati(IV). Humenyuka pamoja na vikaboni iwapo na halijoto kubwa kusababisha athari ya moto. VIKOMO VYA MFIDUO WA KAZI (OELS): TLV: kama Pb 0.05 mg/m³ (kama TWA); A2; BEI imetolewa; (ACGIH 2004). TLV: kama Cr 0.012 mg/m³ (kama TWA); A2; (ACGIH 2004. MAK: Aina ya sarakani: 3B; (DFG 2004). |
NJIA ZA MFIDUO: Dutu hii huweza kufyonzwa ndani ya mwili kwa kuvuta pumzi ya erosoli yake au vumbi na kwa kumeza. HATARI ZA KUVUTA PUMZI: Uvukizi ifikapo 20°C ni kidogo; hata hivyo, ukolezi unaodhuru wa chembechembe zinazopeperuka hewani unaweza kufikiwa haraka wakati wa kunyunyiza au inapotawanywa hasa iwapo katika hali ya poda. ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MFUPI: Dutu hii inakera njia ya upumuaji. ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MREFU AU UNAORUDIWA: Mgusano unaorudiwa au wa muda mrefu huweza kusababisha ugonjwa wa ngozi na vidonda wa muda mrefu. Mgusano unaorudiwa au wa muda mrefu huweza kuhisisha ngozi. Kuvuta hewa kwa kurudia au muda mrefu huweza kusababisha pumu. Mapafu huathirika na mfiduo unaorudiwa au wa muda mrefu. Dutu hii huweza kuathiri damu, uboho, mfumo mkuu wa neva, mfumo wa neva wa pembeni na mafigo kusababisha anemia, madhara kwa ubongo (kama kifafa), ugonjwa wa neva wa pembeni, tumbo kuuma na kuharibika kwa figo. Dutu hii ina uwezekano wa kusababisha kansa kwa binadamu. Inaweza kusababisha kusumisha kwa uzazi na kukua kwa binadamu. | ||
| TABIA ZA KIMAUMBILE | |||
|
Kiwango mchemko (hutengana) Kiwango myeyuko: 844°C Uzito wiani: 6.3 g/cm³ Umumunyifu katika maji, g/100 ml ifikapo 25°C: 0.0000058 |
|||
| DATA YA MAZINGIRA | |||
|
Kuzidisha kwa kemikali yaweza kutokea kwa mfano kufuata mwishono wa vyakula kwa samaki, kwa mimea, kwa mamalia.
| |||
| VIDOKEZO | |||
|
Krometi yaweza kusababisha kansa kwa binadamu, hakuna data za kutosha kuhusu athari za dutu hii. Pigimenti ya krometi risasi yaweza kuwa na kiwango kiasi misombo ya risasi mumunyifu katika maji. Mafusho yenye sumu (misombo ya risasi na kromiamu) hutokea wakati wa kuchomea vyuma, kukata na kukanza vitu vilivyowekewa krometi risasi. Kutegemeana na kiasi cha mfiduo, upimaji wa kitibabu wa mara kwa mara pendekeza. Usichukue nguo za kazi nyumbani. Krometi risasi hutokea kiasili kama madini crocoite, phoenicochroite. Chrome yellow, Cologne yellow, King's yellow, Leipzig yellow, Paris yellow, C.I. Pigment yellow 34, C.I. 77600 ni majina ya kibiashara.
| |||
| MAELEZO YA ZIADA | |||
|
| |||
| |||
| © IPCS, CEC 2005 | |||